Saturday, March 16, 2013

UPONYAJI NA UKOMBOZI KILUVYA - GOGONI

Hall Johnson kutoka nchini Marekani akishirikiana na mwenyeji wake Apostle John Komanya pamoja Mwinjilist John Shabani watahubiri injili na kufanya maombi ya uponyaji kwa wenye shida mbalimbali jijini Dar es salaam.

Wewe mkazi wa Dar es Salaam na mahali pengine popote Tanzania na duniani unakaribishwa.

Friday, March 15, 2013

GOSPEL CELEBRATION CONCERT

Kutakuwa na Tamasha Kubwa la Kusifu na Kuabudu yaani GOSPEL CELEBRATION CONCERT lililo andaliwa na wanafunzi wa Chuo cha Ualimu cha St.Mary`s (ST.MARY`S TEACHER`S COLLEGE) kilichopo Tabata,wakishirikiana na vijana wa kanisa la Dar Calvary Temple (DCT), Jumapili hii ya Tarehe 17/03/2013.

Tamasha hili litaanza saa 11 jioni na kumalizika saa 4 usiku. Hakuna kiiingilio yaani bureee kabisa.

Gospel Celebration Concert litapabwa na Waimbaji wafuatao
Maombezi kwa wenye shida yatafanyika..nyote mnakaribiswa sana!.

KUMBUKA HAKUNA KIINGILIOOOOOOO.

Thursday, March 14, 2013

UZINDUZI WA ALBAM IITWAYO MALIPO TOKA KWA MCH JOSHUA MAKONDEKO

Tarehe 24/3/2013 Jumapili. Waimbaji Sifa John, Masanja Mkandamizaji, Mama Mchungaji Josephin Mwasulama, Joseph Nyuki, Enock Johnasy watakupa nyimbo nyingi zenye kuleta uwepo wa Bwana.

Hii albam iitwayo MALIPO ni albam inayofuata ile ya ZA MWIZI AROBAINI utafanyika pale CITY HARVEST siku ya Jumapili Tarehe 24 March, 2013

Sunday, March 10, 2013

ZIMA UKIMYA NA JESSICA HONORE


Kongamano la Zima Ukimya na Jessica Honore. Hili ni kongamano litakalofanyika ndani ya CITY CHRISTIAN CENTER, Dar es Salaam, Tanzania. Mambo yatakayofanyika katika kongamano la Zima Ukimya na Jesca Honore ni Live Album Sumling, Ministry (The Jessica Music) Preview, Praise and Worship Moment, Uchangishaji fedha kwa ajili ya kununua vifaa vya muziki na mambo mengine  mengi.

Waimbaji waalikwa watakao pamba na kuhudumia kongamano hili ni Miliam Lukindo Wa Mauki pamoja na Upendo Kilahiro, Vocapela, Holy Bass Getor, Doxsaz, Glorious Celebration, R.T.M Bank na wengine wengi




Kwa kiasi kidogo cha fedha ambacho ni shilingi 15,000/= za kitanzania unaweza kuhudhuria kongamano la la Zima Ukimya na Jesca Honore na kupata nafasi ya kushiriki kusongesha mbele kazi ya Bwana na kukutana na wasanii na watu wengine mbalimbali watakao hudhuria kongamano hilo.

Tiketi za tamsha hilo zinapatikana Praise Power Radio na katika kanisa la Word Alive Centre Sinza Mori au unaweza kupiga simu namba hizi 0718 807278 na 0712 332007

Unakaribishwa sana!

Saturday, March 9, 2013

TAMASHA LA KIHISTORIA LILOWAKUSANYA WAIMBAJI WAKONGWE WA ZAMANI NI TAREHE 17/3/2013 KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE

Lile tamasha la kihistori ambalo limewakusanya waimbaji binafsi , kwaya na bendi kongwe sasa zimebakia wiki mbili kuweza kufanyika ni tarehe 17/3/2013 katika ukumbi wa Diamond Jubilee kuanzia saa 7:00 mchana hadi saa 12:00 jioni. Watu  na wadau wa muziki wa injili wanaombwa wasipitwe na tukio jili muhimu bali wajitokeze kwa wingi kuwapa ushirikiano waimbaji wetu wa zamani.

Hili ni Tamasha ambalo limeandaliwa kutambua mchango wa wakongwe wa muziki wa injili Tanzania katika kuinua na kuendeleza muziki wa injili nchini. Baadhi ya wakongwe watakao tumbuiza siku hiyo ni:

Nunu na mumewe Donisi Nkone ambao ni waimbaji wakongwe wa muziki wa injili waishio na kuhudumu nchini Marekani

Upendo Kilahiro ambaye pia ni mkongwe wa muziki wa injili na kipenzi cha watu atashambulia katika jukwaa la Tamasha la wakongwe wa muziki injili

Joge Jabili yule muimbaji bonge wa lulu kwaya ataongoza safu nzima ya mashambulizi ya kwa kwaya ya Lulu Mtoni Kwaya ambayo ni moja ya kwaya kongwe kabilsa nchini Tanzania iliyowahi kutamba na wimbo wao wa Lulu. Kumbuka OOOOO Lulu, OOOOO lulu, OOOOO lulu iko mbinguni!!! Wimbo wa Lulu utapigwa live siku hiyo,

Wakitokea nchini Marekani ambapo wamekaa miezi mingi New Life Band chini ya kiongozi wao HONDO ambaye ni muimbaji na mpiga gitaa la bass katika band hiyo, wataimba live katika Tamasha la wakonwe wa muziki wa injili Tanzania

Pastor Safari ambaye ni mmoja wa waanzilishi wa matamasha ya muziki wa injili Tanzania kutoka DPC Kinondoni pia atashiriki katika Tamasha hili.

Mtaalamu na mtuzi bora wa muziki wa injili Tanzania John Shaban pia atashiriki katika Tamasha hili.